-
-
IBADA: Washarika Azania Front Cathedral Waadhimisha Sikukuu ya Pasaka 2025
Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front tarehe 20 Aprili 2025 ulijumuika na wakristo wote ulimwenguni kusherehekea Sikukuu ya Pasaka. Siku muhimu ya kukumbuka kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Somo: Yesu Mfufuka ni Tumaini la Wote Waaminio ~ Marko 16: 1-8
IBADA: Washarika Azania Front Cathedral Waadhimisha Ijumaa Kuu 2025
Tarehe 18 Aprili 2025 ilifanyika ibada takatifu ya kuadhimisha Siku ya Ijumaa Kuu katika Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front, ibada ambayo iliwakutanisha washarika na wageni mbalimbali ili kukumbuka siku ambayo Yesu Kristo aliteswa na kufa msalabani kabla ya kufufuka siku ya tatu.
Somo: Yesu Alikufa Msalabani Kwa Ajili Yetu ~ Luka 23: 44 - 49
IBADA: Washarika Azania Front Cathedral Waadhimisha Alhamisi Kuu 2025
Katika ibada ya Alhamisi Kuu iliyofanyika katika Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front Cathedral, 17 Aprili 2025 na kuongozwa na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ambaye pia ni Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Baba Askofu Dkt. Alex Malasusa iliwakutanisha washarika na wageni mbalimbali kukumbuka siku ambayo mwokozi wetu Yesu Kristo alisalitiwa na mmoja wa wanafunzi wake aliyejulikana kama Yuda Iskarioti na hivyo kupelekea kukamatwa, kuteswa msalabani mpaka kufa kwake.
-
-
-
-
-
-
Ratiba ya Ibada za Sikukuu ya Pasaka 2025
Hii hapa Ratiba ya Ibada za Sikukuu ya Pasaka 2025 kama ambavyo zitafanyika katika Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front Cathedral.
Washarika, wageni na wananchi wote kwa ujumla mnakaribishwa kujumuika nasi ili tumtukuze Mungu kwa pamoja katika Sikukuu hii muhimu ya Kuteswa, Kufa, Kuzikwa na Kufufuka kwa Bwana Wetu Yesu Kristo.
Wote mnakaribishwa!
Matangazo ya Usharika tarehe 13/04/2025
DAYOSISI YA MASHARIKI NA PWANI
MATANGAZO YA USHARIKA
TAREHE 13 APRILI, 2025
SIKU YA MITENDE
NENO LINALOTUONGOZA NI TUMSHANGILIE BWANA
1. Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli.
2. Wageni: Hakuna Mgeni aliyetufikia na cheti.
3. Matoleo ya Tarehe 06/04/2025
Tunamshukuru Mungu aliyetupa afya ya kumwabudu na utayari wa kumtolea kwa hiari mali alizotupa kwa kazi yake.
NAMBA YA SADAKA KWA NJIA YA MTANDAO:
0757 391174 - KKKT AZANIA FRONT
-
- 1 of 2
- next ›