Kwaya ya Agape Yawafariji Watoto Muhimbili Hospital

Hivi karibuni Kwaya ya Agape inayohudumu katika ibada ya Kiswahili kila Jumapili saa moja asubuhi katika Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front Cathedral iliwatembelea watoto wenye mahitaji mbalimbali katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kuwapa mkono wa faraja.

Watoto walionufaika na ziara hiyo ni wale wenye matatizo ya ugonjwa wa mgongo wazi na wale wenye matatizo ya vichwa vikubwa. Ziara ya kuwatembelea watoto hao ilifanyika tarehe 14/4/2023 ambapo mbali na kupatiwa mahitaji ya siku hadi siku watoto hao pia walipata bima za afya (watoto 100).

AZF | Sikukuu ya Pasaka 2023

Usharika wa KKKT Kanisa Kuu Azania Front Cathedral tarehe 9 Aprili 2023 ulijumuika na wakristo wote ulimwenguni kusherehekea sikukuu ya Pasaka.

Akizungumza katika ibada ya kwanza iliyofanyika Usharikani hapa, Baba Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Dkt. Alex Malasusa alisema sikukuu ya Pasaka ni muhimu sana katika maisha ya mkristo kwani ni kumbukumbu ya kushinda umauti kwa mwokozi wetu Yesu Kristo.

Siku ile ya Ijumaa wafuasi wote wa Yesu waliinamisha vichwa vyao chini kwa sababu Mwalimu wao amekufa alisema Baba Askofu.