MATANGAZO YA USHARIKA TAREHE 9 JUNI, 2019

                                                                    SIKU YA PENTEKOSTE

NENO LINALOTUONGOZA SIKU YA LEO NI

ROHO NDIO MSAADA WETU

  1. Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli.
  2. Wageni: Hakuna mgeni aliyefika na cheti. 
  3. Alhamisi ijayo tarehe 13/06/2019 saa 11.30 jioni kutakuwa na kipindi cha maombi na maombezi. Karibu utupate akili na hekima ya kumjua Mungu. Usikose.
  4. Uongozi wa Usharika unaendelea kuwakaribisha wote kwenye ibada nzuri zinazofanyika kila siku katikati ya wiki hapa usharikani, ibada ya Morning Glory inayoanza saa 12.00 – 1.00 asubuhi, siku ya Jumatatu hadi Ijumaa,  ambayo hukupa fursa ya kuanza kazi na uwepo wa Mungu.  Ibada ya Mchana kila siku saa 7.00 – 7.30 mchana ambayo inakupa nafasi ya kupata faragha  binafsi na Mungu.  Wote mnakaribishwa.
  5. Kesho Jumatatu tarehe 10/06/2019 saa 11.00 jioni Kutakuwa na ibada ya kuenea kwa Roho Mtakatifu. Kwaya zote zitahudumu. Zamu za wazee itakuwa ni kundi la kwanza.
  6. Jumapili ijayo tarehe 16/06/2019 ni siku yetu Maalum ya Harambee ya Kiharaka. Ibada zitakuwa mbili kama kawaida. Ya kwanza itaanza saa 1.00 asubuhi na ya pili itaanza saa 4.00 asubuhi. Washarika tuiombee siku hiyo. Aidha Vitenge vya Kiharaka vipo kwa bei ya sh. 10,000/=.  Vitenge hivi ndiyo sare siku ya Harambee kwa Washarika wote.
  7. NDOA

NDOA ZA WASHARIKA

Kwa mara ya Kwanza tunatangaza ndoa za tarehe 29.06.2019

SAA 7.00 MCHANA

Bw. Mussa Mayala Masala              na     Bi. Maryrose Jacob Mtei

SAA 10.00 JIONI

Bw. Baraka Adon Francis               na     Bi. Brenda Joseh Korassa

Kwa mara ya Pili tunatangaza ndoa za tarehe 22.06.2019.

SAA 9.00 ALASIRI

Bw. Richard Absalum Mpogole       na     Bi. Janeth Daniel Mgaliwa

Ndoa hii ifuatayo itafungwa KKKT Kanisa Kuu Njombe kati ya

Bw. Ephrahim Yohana Sanga         na     Bi. Neema Aston Kibona

 

Matangazo mengine ya ndoa yamebandikwa kwenye ubao matangazo.Karibu na duka letu la vitabu

  1. IBADA ZA NYUMBA KWA NYUMBA

          Wazo/Tegeta/Kunduchi/Bahari Beach/Ununio: Kwa Bwana na Bibi Kevela

          Mwenge/Kijitonyama/Makumbusho/Sinza/Ubungo/Makongo: Kwa Bi. Mary Kinisa

    Mjini kati: Kwa mama Mongi

    Ilala/Chang’ombe/Mivinjeni: Kwa Dr. na Bibi D. Ruhago

    Kawe/Mikocheni/Mbezi Beach: Kwa Bwana na Bibi T. Msangi

   Tabata: Kwa Bwana na Bibi J. Mwakasege

   Oysterbay/Masaki:  

   Upanga: kwa Bwana na Bibi Nkya – (Mariki Road)

   Kinondoni: Kwa Prof. G. Mmari

 

Zamu: Zamu za wazee leo ni kundi la Kwanza

 

Na huu ndio mwisho wa matangazo yetu, Mungu ayabariki.