Azaniafront Cathedral - Tamasha la Uimbaji 2021

Siku ya Jumapili, 30/5/2021, lilifanyika tamasha la uimbaji ambalo lilishirikisha kwaya sita zinazohudumu katika Usharika wa Kanisa Kuu Azaniafront Cathedral chini ya usimamizi wa Kamati ya Uinjilisti ya usharika ikiongozwa na mwenyekiti wake Mzee Simon Jengo.

Mbali ya uimbaji, tamasha hilo liliambatana na semina iliyofunguliwa na Mchungaji Joseph Mlaki aliyefundisha juu ya asili ya uimbaji akitumia somo kutoka katika kitabu cha Zaburi 146:1-2. Mchungaji Mlaki aliwaasa waimbaji kuimba kwa furaha na kwa kumsifu Bwana.