Date: 
26-06-2026
Reading: 
Yoshua 23:1-11

Ijumaa asubuhi tarehe 26.06.2026

Yoshua 23:1-11

1 Hata ikawa baada ya siku nyingi, Bwana alipokuwa amekwisha kuwapa Israeli raha mbele ya adui zao pande zote, naye Yoshua alipokuwa mzee, mwenye miaka mingi sana,

2 Yoshua akawaita Israeli wote, wazee wao, na wakuu wao, na makadhi yao, na maakida yao, akawaambia, Mimi ni mzee, nami nimekwendelea sana katika miaka yangu;

3 nanyi mmeona mambo yote ambayo Bwana, Mungu wenu, amewatenda mataifa haya yote kwa ajili yenu; kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye aliyewapigania ninyi.

4 Tazama, nimewagawieni kwa kura mataifa haya yaliyobaki, yawe urithi kwa kabila zenu, toka mto wa Yordani, pamoja na mataifa yote niliyowakatilia mbali, mpaka bahari kubwa upande wa machweo ya jua.

5 Yeye Bwana, Mungu wenu, atawatoa kwa nguvu mbele yenu, atawafukuza wasiwe mbele ya macho yenu tena; nanyi mtaimiliki nchi yao, kama Bwana Mungu wenu, alivyowaambia.

6 Basi, iweni mashujaa sana kuyashika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati ya Musa, na kuyatenda, msiyaache kwa kugeukia upande wa kuume wala upande wa kushoto.

7 Msiingie kati ya mataifa haya, yaani, haya yaliyobaki kati yenu; wala msitaje majina ya miungu yao, wala kuwaapisha watu kwa majina hayo, wala kuitumikia, wala kujiinamisha mbele yao;

8 bali shikamaneni na Bwana, Mungu wenu, kama mlivyotenda hata hivi leo.

9 Maana Bwana amefukuza mbele yenu mataifa walio hodari, kisha wenye nguvu, lakini kwenu ninyi hapana mtu aliyesimama mbele yenu hata leo.

10 Mtu mmoja miongoni mwenu atafukuza watu elfu; maana Bwana, Mungu wenu, ndiye anayewapigania, kama alivyowaambia.

11 Jihadharini nafsi zenu, basi, ili mmpende Bwana, Mungu wenu.

Pamoja tujenge Kanisa la Bwana;

Yoshua akiwa anawaongoza Israeli kuelekea nchi ya ahadi baada ya Musa, anawaambia kwamba sasa yeye ni mzee, na kuwakumbusha kuwa Bwana ndiye aliyewapigania. Anawapa uhakika wa kuimiliki nchi kama walivyoahidiwa na Bwana. Anawasihi kuachana na miungu, kushikamana na Bwana.

Ujumbe wa Yoshua kwa wana wa Israeli ulikuwa ni kumtegemea Bwana aliyewapigania, wakimpenda na kumtumikia. Ndiyo ujumbe tunaopewa asubuhi ya leo, kumtegemea Yesu Kristo aliyetuokoa, na kumtumikia siku zote za maisha yetu. Tutende yote hayo kwa umoja, ndipo tutalijenga Kanisa la Bwana. Amina

Siku njema

Heri Buberwa