Matangazo ya Usharika tarehe 5 Novemba 2023

MATANGAZO YA USHARIKA 

TAREHE 05 NOVEMBA, 2023

SIKU YA KUKUMBUKA WATAKATIFU

NENO LINALOTUONGOZA SIKU YA LEO NI

UENYEJI WA MBINGUNI

1.Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli. 

2. Wageni: Hakuna mgeni aliyetufikia kwa cheti. 

3. Matoleo ya Tarehe 29/10/2023

Tunamshukuru Mungu aliyetupa afya ya kumwabudu na utayari wa kumtolea kwa hiari mali alizotupa kwa kazi yake.

NAMBA YA SADAKA KWA NJIA YA MTANDAO:

AZF | Sikukuu ya Mavuno 2023: "Sikukuu Kamili ya Kanisa ya Utoaji" - Dean Chediel Lwiza

Siku ya Jumapili, tarehe 22/10/2023, KKKT -DMP Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front Cathedral ulifanya maadhimisho ya kilele cha sikukuu ya mavuno ya mwaka 2023, maadhimisho ambayo hufanyika kila mwaka ili kutoa fursa kwa washarika kumtolea Mungu sehemu ya matunda au mavuno ya kazi walizozifanya kwa kipindi cha mwaka mzima.

Ibada ya kusherehekea sikukuu hii ya mavuno kwa mwaka huu imefanyika katika viwanja vya usharika wa Kanisa Kuu Azania Front Cathedral huku ikihudhuiriwa na mamia ya washarika waliojitokeza kwa wingi wakiwa na mavuno yao tayari kwa kumtolea Mungu.