Hayo yalikuwa ni maneno ya kichwa cha habari katika semina ya kiroho ya umoja wa

wanawake wa usharika wa Azania Front iliyofanyika kule Belinda Beach Resort siku ya

jumamosi tarehe 14/6/2014.

Wengi wamekuwa na fikra kwamba mwanamke kazi yake ni kulea watoto nyumbani tu,

kumbe mwanamke ana kazi nyingi ambazo ndiyo majukumu yake yampasayo kuyatenda

kila siku, kwa kifupi naweza kusema huo ni upako wa kipekee ambao mwanamke amepewa

na Mungu, kwani mungu ana mpango na kila mwanamke anayemtumikia. Pia wanawake wana

nafasi katika maombi ya kuiombea familia, kanisa na nchi. Ukiangalia kwa maisha ya kila siku,

mwanamke ndio wa kwanza kuamka na ndio wa mwisho kulala.“Wanawake wana nafasi ya kipekee

katika kanisa na niwashauri katika familia, hivyo basi wastahili kupewa nafasi ya kusikilizwa maana

mchango wao ni muhimu sana katika jamii” alisema Chaplin Charles Mzinga alipokuwa anafungua

semina ya kiroho ya siku moja iliyofanyika mjini Dar es salaam.

“Wanawake siku zote ndio wanaotetea familia, ndio maana Yesu aliwaambia wanawake kwamba,

msinililie mimi bali lieni kwa ajili ya familia zenu na watoto wenu, ukisoma kwa makini utaona

kwamba wanawake ndio waliokuwa wanapewa kipaumbele katika kila kitu, pia wanawake ndio

waliokuwa wa kwanza kujua kwamba Yesu amefufuka kutoka kaburini, inaonyesha jinsi gani

mwanamke ana nafasi katika maisha ya kila siku ya mwanadamu ” alisema Chaplin Charles Mzinga.

Naye Mnenaji katika semina hiyo Mchungaji Grace Masalakulangwa alisema’Mungu ameweka mambo

matano makubwa ya uelewa ndani ya mwanamke nayo ni ,

¦

1.Kipawa cha ushawishi na ushauri.

2.Hali ya kuthubutu ,

3.Kutatua matatizo na kutia moyo na kupatanisha

4.Uombolezaji

5.kuhakiki ustawi wa kiuchumi katika familia. 

¦

belinda201

Baadhi ya wanawake wakifatilia jambo kwenye semina

¦

belinda202

Chaplain Charles Mzinga akifungu Semina ya Wanawake wa Azania Front

¦

belinda205

Katibu Mkuu wa umoja wa wanawake wa Azania Front akiongea jambo wakati wa semina

¦

belinda207

Khanga ya kumbukumbu ya Semina ya Wanawake iliyofanyika Belinda Resort mwaka 2014

¦

belinda209

Makamu Mwenyekiti Bi Stella Sykes (kushoto) na Katibu Msaidizi Bi Jane Mhina wakifuatilia maombi

¦

belinda211

Mama Askofu Erica Malasusa akielekea meza kuu kwenda kmkaribisha mgeni rasmi

¦

belinda212

Mama Mchungaji T Kibona (kulia) akiwasalimu wanasemina

¦

belinda213

Mchungaji, Mnenaji G. Masalakulangwa akiliombea kanisa na Taifa la Tanzania

¦

belinda217

Msehereshaji Mama A Mzinga akisisitiza jambo

¦

belinda219

Mshereheshaji wa nyimbo za kusifu na kuabudu Paul Mwangosi, akitumbuiza katika Semina

¦

belinda221

Mwanasemina Bi kavugha, akiwaasa wanawake na wasichana katika semina

¦

belinda222

Mwasibu wa Umoja wa Uanawake Bi Elly Swai akijiandaa na semina

¦

belinda226

Mwenyekiti Bi A kilewo akiwatambulisha viongozi wa Umoja wa wanawake wa Azania Front

¦

belinda228

Viongozi wa Azania Front wakiwa na wageni rasmi katika picha ya pamoja

¦

belinda232

Wakinamama wa kwaya ya Wanawake wa Azania Front wakiimba

¦

belinda237

Wanasemina wakiomba

¦

belinda240

Watoto wa kike waliohudhuria semina wakiombewa