Waalimu wa Shule ya Jumapili Azaniafront wapigwa msasa

Waalimu wa shule ya Jumapili ya Usharika wa Kanisa Kuu Azaniafront, hivi karibuni walihudhuria semina iliyoandaliwa na usharika na kufanyika siku ya Jumamosi tarehe 31/10/2020. Semina hiyo ilishirikisha walimu wa usharikani pamoja na walimu wa Shule za Jumapili kutoka katika mitaa inayotunzwa na Usharika wa Kanisa Kuu, mitaa hiyo ni pamoja na Viwege, Dondwe, Mvuti na Tabora.

Sikukuu ya Mavuno - 2020

KKKT Azaniafront yaadhimisha ‘Sikukuu ya Mavuno’ kwa mwaka 2020

Siku ya Jumapili, tarehe 25/10/2020, Usharika wa KKKT Kanisa Kuu la Azaniafront ulifanya maadhimisho ya sikukuu ya mavuno, sikukuu ambayo hufanyika kila mwaka kwa washarika kumtolea Mungu sehemu ya matunda ya kazi wanazozifanya.

Ibada ya kusherehekea sikukuu hii ya mavuno kwa mwaka 2020 ilifanyika katika viwanja vya usharika wa Kanisa Kuu Azaniafront huku ikihudhuiriwa na washarika waliojitokeza kwa wingi wakiwa na mavuno yao tayari kwa kumtolea Mungu.