Ni siku maalumu iliyokuwa inangojwa kwa hamu kubwa na ya kipekee kwa Kwaya Kuu ya Azania Front, ni tarehe 7 Septemba

2014 ya kuzindua mkanda wao vol. ya tisa (9). Kikundi kiliingia kanisani asubuhi kikiongozwa na Mwalimu mzoefu na wa siku

nyingi Abisai Faragha mpiga kinanda na mfundishaji wa nyimbo za noten au nyimbo sanifu, Kwaya ilingia Ibada ya kwanza,

na hatimaye Ibada ya pili na kuanza uimbaji moja kwa moja kutegemea na liturgia iliyokuwa ikiongozwa na Mchungaji Kiongozi

-Chaplain Charles Mzinga.

Kanda ilizinduliwa katika Ibada zote na iliambatana na maombi maalumu ya kuiombea kwaya ili kanda iweze kuleta utukufu

hata kwa msikilizaji. Kwaya ilifanya vizuri na ilileta msisimko mkubwa sana, na katika nyimbo mbili zilizoimbwa watu

walizipokea vizuri na haikuwa kazi kubwa hata kwa Mchungaji alipoita watu kuja kununua au kuchangia kwaya kwenda mbele

kutoa bila matatizo. Na hii ndio Risala iliyotangulia kusomwa na Mlezi wa Kwaya Kuu Mama Elipina Mlaki ambaye sasa ni

Mzee wa Kanisa. Alisoma kwa makini na weledi wa hali ya juu. Bofya hapa kusoma risala....

Kwaya Kuu imepokea vingozi wapya wa kikundi mwaka huu baada ya uchaguzi 2014 ambao ni

-Â - Elisha Mushumbusi - Mwenyekiti

-Â - Suzan Muro Towo - Makamu Mwenyekiti

-Â - Grace Makalla - Katibu

-Â - Margreth Godwin - Katibu Msaidizi

-Â-- Heri Nteboya - Mtunza Hazina

-Â-- Edward Mkony - Mtunza Hazina Msaidizi

-Â - Mwl Abisai Faragha - Mwalimu Mkuu wa kwaya

Tunamshukuru Mungu kwa ajili yao na tunawaombea kwa Mungu wasichoke njiani na waweze kuifanya kazi ya Mungu kwa

uaminifu na mafanikio injili isonge mbele.

Jumuisho

Mwalimu, Viongozi na wanakwaya kwa ujumla wanapenda kuwashukuru watu wote kwa ushirikiano mzuri waliouonyesha

kipindi chote cha maandalizi na kufanikisha zoezi zima la Uzinduzi. Na wale waliotoa mali zao Muda wao na yote.

MUNGU WETU ALIYE HAI AWABARIKI SANA.

kkuu1

Mmoja wa walezi wa Kwaya Kuu Mama E. Mlaki akitoa maelezo mafupi kwa washarika siku ya uzinduzi wa mkanda Vo. 9 kwa niaba ya

wanakwaya kuu na walezi Tar 7 Septemba 2014.

kkuu2

Kwaya Kuu wakiwa katika Ibada siku ya uzinduzi wa kanda Vo. 9 Tarehe 7 September 2014

kkuu13

Kwaya kuu wakionesha na kuimba siku ya uzinduzi katika ibada wakiongozwa na Mwl Abisai Faragha.

kuimba1

Wanakwaya Kuu Azania Front wakiimba wakati wa Ibada siku ya uzinduzi.

kuimba2

Doscar Vuhahula na Mama Anna Kavugha wakiwa katika uimbaji siku ya uzinduzi.

kuimba3

Isabela Hingi na Doscar Vuhahula wakiwa katika uimbaji siku ya uzinduzi.

kuimba5

Mwl Abisai Faragha akiongoza kwaya wakati wa ibada siku ya uzinduzi

kuimba6

kkuu12

Mchungaji Charles Mzinga akifanya maombi baada ya wanakwaya kuimba siku ya uzinduzi Azania Front na kubariki kanda vo. 9.

kkuu3

Mzee Buchanagandi (Mzee wa kanisa)akichangia kwa kununua kanda siku ya uzinduzi.

kuimba4

 

kkuu4

Mzee Minja wa kwaya ya Upendo Azania Front akimnunulia mke wake kanda siku ya uzinduzi.

kkuu5

Mzee George Mnyitafu, mmoja wa walezi wa Kwaya akinunua kanda siku ya uzinduzi.

kkuu6

Baadhi ya waimbaji wakichangia kwaya yao kwa kununua kanda Doscar Vuhahula na anayefuata Mama Omega Mongi.

kkuu7

Mama E. Mlaki Mlezi wa kwaya Kuuu akinunua kanda siku ya uzinduzi.

kkuu8

Kwaya kuu Azania Front wakiwamalizia ibada nje baada ya uzinduzi.

kkuu9

Mwenyekit i wa Kwaya Kuu Azania Front Bw. Elisha Mushumbusi akisalimiana na mmoja wa walezi wa kwaya Kuu Mzee Benjamin Mpamo

baada ya ibada ya Uzinduzi.

kkuu10

Kutoka kushoto Ni mama Anna Kavugha, Erica Byabato na Waeli R. Koshuma waimbaji wa muda mrefu katika kwaya kuu ya Azania Front.

Mama Anna ameimba kwa miaka 54 mpaka sasa na Mama Waeli ameimba kwa Miaka 58 mpaka sasa!

kkuu11

Baada ya uzinduzi viongozi wa kwaya Kuu wakihesabu walichokusanya siku ya uzinduzi.

kkuu14

Mmoja wa washarika wa Azania Front Mzee Kida akichangia kwa kununua kanda ya kwaya siku ya uzinduzi 7 septemba 2014 akisindikizwa na

Mama C. Nzali mwimbaji kwaya kuu.

kkuu15

Mzee Adam Mpanda mmoja wa wanakwaya kuu akinunua kanda ya kwaya kuu siku ya uzinduzi.

kkuu16

Mama Waeli Koshuma Kushoto na Mama Anna Kavugha Kulia wakiombewa na Mch C. Mzinga baada ya kutoa shukrani ya pekee kwa jinsi Mungu

alivyowajalia kumtumikia kwa njia ya uimbaji tangu wakiwa wasichana mpaka leo. Mama Anna kwa Miaka 54 na Mama Waeli kwa mika 58.

Pembeni ni Mwenyekiti wa kwaya kuu akushuhudia tendo hilo.