Event Date: 
28-09-2014

Tukio hilo lilifanyika kanisani Azania katika ibada zote 2 za kiswahili likiongozwa na Msaidizi wa Askofu Dean

George Fupe akisidiana na Chaplain Charles Mzinga. Kabla ya harambee, video fupi inayoonyesha maendeleo

ya mradi ulipofikia ilionyeshwa. Chaplain Mzinga alisema lengo la harambee hiyo ni kukusanya jumla ya

Shilingi 300 milioni ili kufikia bajeti ya Sh. 700 milioni zinazohitajika kukidhi zoezi lakuezeka paa la jengo la

mikutano, ambalo ndio awamu ya kwanza ya mradi. Aidha paa hilo la iana yake, litatengenezwa China na kuja

kuunganishwa kwenye jengo Kiharaka. Pia kitenge maalum kwa ajili ya kuchangia mradi kiliwekwa wakfu na

Dean Fupe, na kunadiwa. Ushiriki wa washarika ulikuwa mzuri, wote walipewa nafasi yakushiriki kwa jinsi nafsi

zao zilivyowasukuma. Pia tulibarikiwa sana namahubiri ya Mch. Richard Hanaja wa KKKT Kigogo, aliyetoa mahubiri

ya siku hiyo. Kichwa cha Neno kilikuwa "Utoaji wa Kikristo" 2 Wakorintho 1-5 

harambeeasb01

Dean Fupe akizindua harambee katika ibada ya kwanza

harambeeasb02

Wazee wa usharika waliokuwapo waliongoza kutoa ahadi zao katika ibada ya kwanza.

harambeeasb06

Washarika wa ibada ya kwanza wakifuatilia harambee kwa makini

harambeeasb09

Kitenge maalum kiliwekwa wakfu na kunadiwa

harambeeasb10

Msharika wa kwanza kununua kitenge kwa mnada.

harambeeasb12

Mzee wa usharika, Dr. Samwel Swai naye akipata kitenge.

harambeeasb13

Chaplain Mzinga akinadi kitenge

harambeeasb18

Wengi walichangamkia fursa ya kupata kitenge maalum.

harambeeasb08

Wazee Gody na Beatrice wakiwa katika kuweka mahesabu sawa huku harambee ikiendelea.

______________________________________________________________________________________________________________

Katika ibada ya pili, kwa sehemu mambo yalikuwa hivi...

harambee201

Dean Fupe akihamasisha harambee

harambee203

Injinia Kishimbo na mkewe wa KKKT Kijitonyama wakituunga mkono kwenye harambee.

harambee204

Washarika H. Moshi na mkewe wakichangia

harambee206

Mzee E. Moshi na Mama Mengi wakichangia harambee

harambee208

harambee211

Mzee T. Mlaki "mzee wa kiharaka" akichangia na wengine wakisubiri zamu yao.

harambee217

harambee225

Walikuwepo watu wa rika zote.

harambee229

harambee235

Mch. mstaafu Aston Kibona alikuwepo

harambee241

Doris, Katibu wa Chaplain naye alikuwapo

harambee249

Chaplain Mzinga akinadi Kitenge maalum ibada ya pili

harambee238

Mzee Filemon Mgaya akichangia

harambee271

Msharika akipata kitenge