MATANGAZO YA USHARIKA

TAREHE 19 MACHI, 2023

NENO LINALOTUONGOZA SIKU YA LEO NI

YESU NI CHAKULA CHA UZIMA

1. Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli.

2. Wageni: Hakuna mgeni aliyetufikia kwa cheti.

3. Matoleo ya Tarehe 12/03/2023

    Tunamshukuru Mungu aliyetupa afya ya kumwabudu na utayari wakumtolea

    kwa hiari mali alizotupa kwa kazi yake.

NAMBA YA SADAKA KWA NJIA YA MTANDAO:

- 0757 391174 - KKKT AZANIA FRONT

- Namba ya Wakala M-PESA – 5795794 – KKKT AZANIA FRONT

CATHEDRAL

4. Tunapenda kuwakumbusha na kuwakaribisha wote katika ibada zetu siku za

     jumapili Ibada ya kwanza, inayoendeshwa kwa lugha ya Kiswahili, inayoanza

     saa 1:00 asubuhi; Ibada ya pili, inayoendeshwa kwa Kiingereza, inayoanza

     saa 3:00 asubuhi; Ibada ya tatu, inayoendeshwa kwa Kiswahili, inayoanza saa

     4:30 asubuhi. vipindi vya kujifunza neno la Mungu hapa Usharikani kila siku

     za juma. Morning Glory saa 12.00 asubuhi ili kuanza siku kwa Uongozi wa

     Mungu, Ibada za mchana saa 7.00 -7.30 mchana tunapopata faragha binafsi

     na Mungu. Alhamisi jioni saa 11.00 jioni tuna kipindi cha Maombi na

     Maombezi, ambapo tunajifunza neno la Mungu na kupata muda wa kutosha

      wa maombi. Vipindi vyote vinarushwa Mubashara kupitia Azania Front TV.

      Karibu.

5. Ratiba yetu ya mafundisho katika msimu wa Kwaresma hapa Kanisa Kuu,

     inaendelea. Na kwa wiki hii ya tarehe 12 hadi 18 Machi tutakuwa na

     A. Ibada ya Majivu siku ya Jumatano, na

     B. Semina ya Neno la Mungu kuanzia hiyo J5 tarehe 22 hadi Ijumaa tarehe 24

         Machi 2023.

     Semina zetu za Kwaresma zitaendelea kama zilivyopangwa hadi mwisho wa

     msimu tarehe 31 Machi 2023. Vipindi vyote vinaanza saa 11:00 jioni. Karibuni

     wote tumfanyie Mungu Ibada njema.

6. Leo tarehe 19/03/2023 mara baada ya ibada tutakuwa na Mkutano Mkuu wa

    Usharika.

7. Uongozi wa Umoja wa Wanawake unapenda kuwakumbusha wale wote

    waliochukua kadi za kuchangia ada za watoto Yatima ambao bado

    hawajarudisha au kukamilisha ahadi zao waweze kukamilisha ifikapo tarehe

    31 Machi 2023. Tunatanguliza shukrani kwa sadaka zenu kwa ajili ya watoto

    hao. Mungu awabariki.

8. Jumamosi ya Tarehe 01/04/2023 saa 3.00 asubuhi kutakuwa na ibada ya

    wazee kuanzia miaka 60. Washarika tuendelee kuiombea siku hiyo.

9. Jumamosi ijayo tarehe 25/03/2023 saa 3.00 asubuhi mpaka saa 7.00 mchana

    hapa usharikani Azania Front Cathedral kutakuwa na Semina ya Wajane na

    Wagane. Mnenaji atakuwa ni Mama Hevenlight Swai kutoka usharika wa

    Kariakoo. Wote mnakaribishwa.

10. Jumapili ijayo tarehe 26/03/2023 tutashiriki Chakula cha Bwana. Washarika

      Tujiandae.

11. IBADA ZA NYUMBA KWA NYUMBA

  • Oysterbay na Masaki:/ Mikocheni, Kawe, Mbezi Beach Watashiriki

           ibada hapa Usharikani

  • Makumbusho, Kijitonyama, Sinza, Mwenge, Makongo na Ubungo:

          Kwa Mama Ruth Korosso

  • Mjini kati: Hapa Usharikani Jumamosi saa 1.00 asubuhi
  • Ilala, Chang’ombe na Buguruni: Kwa Dada Christina
  • Kinondoni: Kwa Mama Hilda Lwezaula
  • Tegeta, Kunduchi, Bahari Beach, Ununio: Kwa …………..
  • Upanga: Kwa Bwana na Bibi George Kinyaha Alykhan road
  • Tabata: Kwa Mch. Aston Kibona

12. MAHUDHURIO YA IBADA - TAREHE 12/03/2023

       Jumla ibada zote watu ….. 710

 13. Zamu: Zamu za wazee ni Wazee wote watakuwa zamu

       Na huu ndiyo mwisho wa matangazo yetu, Bwana ayabariki.