Wenza wa Wachungaji DMP watoa shukrani

Wenza wa wachungaji wa KKKT Sharika za Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP) wametoa shukrani katika Usharika wa Kanisa Kuu Azaniafront Cathedral kama sehemu ya kuadhimisha miaka nane tangu kuanzishwa kwa vicoba ambayo mpaka sasa ina akiba ya takriban Tsh 400,000,000/-. Pia vicoba hiyo hivi karibuni imechaguliwa kuwa vicoba bora katika nyanja ya uwekezaji nchini Tanzania.

Sikukuu ya Mikael na Watoto 2021

Wazazi waaswa kuwalea watoto katika msingi wa neno la Mungu

"Tuwapende na tuwajali watoto wetu," hayo ni maneno ya kutoka katika Biblia yaliyotumika katika mahubiri yaliyofanyika katika ibada ya Sikukuu ya Mikael na watoto iliyofanyika siku ya Jumapili tarehe 3 Oktoba 2021 katika Usharika wa Kanisa Kuu Azaniafront.