KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA

DAYOSISI YA MASHARIKI NA PWANI

MATANGAZO YA USHARIKA

LEO TAREHE 30 OKTOBA, 2016

NENO LINALOTUONGOZA SIKU YA LEO NI USHUHUDA WETU

  1. Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli.
  1. Wageni: Wageni waliotufikia na Cheti ni.

         Kama kuna wageni wengine walioshiriki nasi wasimame ili tuwakaribishe.

  1. Leo tutashiriki Chakula cha Bwana. Washarika karibuni.
  1. Jumapili ijayo tarehe 06/10/2016 tutamtolea Mungu fungu la kumi. Washarika tujiandae. Wazee watagawa bahasha.
  1. Alhamisi ijayo tarehe 03.11.2016 saa 11.00 jioni kutakuwa na maombi na maombezi yatakayoongozwa na mtumishi Sweetbert Lugemalila.  Wagonjwa na wenye shida mbalimbali pia watapata huduma siku hiyo. Wote mnakaribishwa na muwaarifu na wengine.
  1. SHUKRANI

Jumapili ijayo tarehe 6.11.2016 familia nne (4) zitatoa shukrani

Ibada ya Kwanza.

  • Mama Miriam Luhui atamshukuru Mungu kwa Mambo mengi mema aliyomtendea ikiwa ni pamoja na kufikisha miaka 80.

Neno: Zab. 116:1-2

Wimbo: Yesu ni rafiki wa kweli (Kwaya ya Upendo)

Ibada ya Pili

  • Familia ya Kaduri watamshukuru Mungu kwa mambo mengi aliyotendewa katika familia yao ikiwa ni pamoja na Mama Anna Kaduri kufikisha miaka 70

Neno:

Wimbo: Zawadi gani nitamtolea Bwana (Kwaya ya Vijana)

  • Familia ya Mama Aida Mwakisu nao watamshukuru Mungu kwa mambo mengi aliyowatendea pamoja na Mama Aida Mwakisu kufikisha miaka 60 na kustaafu salama.

Neno: Zab. 138

Wimbo: Niende wapi nijiepushe na uso wako Mungu (Ataimba mwenyewe), Ee Mungu wangu (Kwaya ya Umoja)  

  • Mzee Evatt Kuzilwa atamshukuru Mungu kwa kumaliza msiba salama wa mke wake Anna Kuzilwa na kuendelea kumtunza na Kumtia nguvu. 

Neno: Zab. 71:16-19

Wimbo: (Na. 331) Nivute kwa Bwana Yesu, Huniongoza Mwokozi                                                                           (Kwaya Kuu)   

  1. NDOA:

NDOA ZA WASHARIKA

KWA MARA YA KWANZA TUNATANGAZA NDOA ZA TAREHE 19.11.2016

SAA 8.00 MCHANA

Bw. Ronald Justo Mbowe          na     Bi. Upendo Gilliaara Nkini

Ndoa ifuatayo itafungwa Katoriki Parokia ya Tagaste Chekereni Parish kati ya

Bw. Joachim Heven Meena       na     Bi. Prisca Said

 

TAREHE 20.11.2016

SAA 7.00 Mchana

Bw. Erick Rwemanya Lutahakana      na     Bi. Hellen Fredrick Fungamtama

 

KWA MARA YA PILI TUNATANGAZA NDOA ZA TAREHE 12.11.2016

SAA 10.00 JIONI

Bw. Eric Siddon Mosha             na     Bi. Akarii Abdallah Godigodi

Matangazo mengine ya Ndoa yamebandikwa kwenye ubao wa matangazo karibu na duka letu la vitabu

 

  1. Ibada za Nyumba kwa Nyumba
  • Upanga: Bwana na Bibi H.  Nkya
  • Kinondoni: Kwa Bwana na Bibi T. Onesmo
  • Ilala/Chang’ombe/Mivinjeni: Kwa Bwana na Bibi Kowero
  • Kawe/Mikocheni/Mbezi Beach: Bibi Happiness Chamungwana
  • Oysterbay/Masaki: Watatangaziana
  • Tabata: Kwa Mchungaji Kibona
  • Kijitonyama/Sinza/Mwenge/Makumbusho/Ubungo: Watatangaziana
  • Mjini kati: Watatangaziana
  • Wazo/tegeta/Kunduchi/BahariBeach/Ununio:  Kwa Bwana na Bibi Peter Mlagha

 

Zamu: Zamu za wazee ni kundi la Kwanza

Na huu ndio mwisho wa matangazo yetu, Mungu ayabariki  

 

 

 

 

ZAMU ZA WAZEE

IBADA YA I

MZEE CUTHBERT SWAI               -        NENO LA WARAKA   - Rum. 3:19-20

                                                                   NENO LA PILI         - Yn. 2:13-17

MZEE  JOHN MKONY                   -        MATANGAZO

 

IBADA YA II

MZEE DORIS MARO                     -        NENO LA WARAKA   - Rum. 3:19-20                                                                                                NENO LA PILI          -  Yn. 2:13-17

MZEE ELIHURUMA NANGAWE       -        MATANGAZO